Kuna habari za kuaminika kuwa Mhe Rostam Aziz maarufu humu kama RA amekuwa akihaha katika vyumba vya habari na kufanya vikao mbalimbali na baadhi ya wahariri na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari nchini kumtengenezea mabomu Zitto Kabwe ili jamii iache kuamini kile ambacho amekuwa akikisimamia katika siku za hivi karibuni.

Kumbukeni kuwa RA ndiye alikuwa mmoja wa wakuu wa idara ya propaganda wakati wa kampeni za urais ndani ya CCM mwaka 2005. Kwa kutumia waandishi mbalimbali ambao wengi wao tayari wameshatajwa hadharani huyu jamaa ndiye alikuwa chanzo cha habari nyingi nyeti za serikali ambazo zilipelekea kuanguka kisiasa kwa mawaziri kadhaa wa serikali ya tatu ambao walikuwa wakonekana tishio kwa JK ambaye walitegemea kupata ride yake kuneemesha maslahi yao binafsi.

Huyu jamaa ambaye kwa sasa ndio anaonekana kama KING MAKER nchini mwetu na kiongozi wa pili katika kundi la MTANDAO MASLAHI akifuatiwa na mshirika wake kibiashara na tajiri mwenzake Nizar Karamagi amekuwa mwiba mkubwa kwa JK kutokana na uroho wake wa kutaka awe katika kila deal inayoendelea nchini. Rostam ni mtu mwenye upeo mkubwa sana wa kiakili na mjanja kibiashara na asiye na simile katika kulinda maslahi yake. Mbinu chafu ndio jina lake la pili na unafiki ndio middle name yake.

Katika hali inayojitokeza sasa inaelekea RA anapigania maslahi ya kundi ziima la MTANDAO MASLAHI kutokana na dalili kuwa limekuwa mzigo mzito kwa JK kufikia mahala kuonyesha dalili zote za kushukiwa na nyundo kali hata kabla ya uchaguzi wa ndani wa chama kufanyika.

Pamoja na kuwa maslahi katika makampuni mbalimbali miliki ya vyombo vya habari kama Habari Corporation ambayo hutoa magazeti ya RAI, MTANZANIA na vilevile share ndogo katika umiliki wa gazeti la MWANANCHI na THE CITIZEN ambako amekuwa akizidiwa nguvu na Wakenya, RA anaushawishi mkubwa kwa waandishi wengi wa magazeti yetu kufikia wakati fulani kuwa akiwalipa mishahara tena mikubwa kuliko wapatayo kutoka kwa waajiri zao.

Moja ya kazi inayoendelea ni uandishi wa makala mbalimbali za kuwahadaa watanzania kutomuamini Zitto kabwe akiwatumi watu kaka Dr Gideon Shoo na Muhingo Rweyemamu ambao kwa miaka mingi sasa wamekuwa watumishi wake waaminifu katika kazi ya UHANDISI WA HABARI. Hawa ni vinara tu lakini wapo wengi wengine. ngome yake nyingine ni Gazeti la MAJIRA.

Kwa hali inayoendelea ni wazi mtasikia mengi kuhusu Zitto Kabwe lakini kuweni makini na kujaribu kujua vyanzo vya habari hizo. cha ajabu ni kuwa huyu jamii wakati wote hupenda kujifanya ni rafiki wa Zitto na kujigamba kuwa anamkubali na misimamo yake lakini ukweli ni kuwa akipata nafasi tu hataacha kummaliza ndugu yetu na kijana mwenzetu Zitto Kabwe. Ukweli ni kuwa RA ameshiriki hata kupanga njamaa za kuwaundermine baadhi ya wanamtandao wenzake ambao wanonekana kuelemea kundi la MTANDAO MATUMAINI linaloongozwa na Waziri MMoja mwandamizi Nchini ambalo liliweka imani ya matumaini ya watanzania kwa JK ambaye anaonekana kuelemewa nguvu na mafisadi waliojikita katika mpango wa kula hadi kusaza utajiri wa watanzania.

Zaidi sintashangaa kuwa hili likawa kosa la mwisho la RA ambalo sio tu litamrudi yeye binafsi lakini pia lina hatari ya kuzua hasira za watanzania wengine dhidi ya watanzania wenzao wenye asili ya asia (mnapenda waita wahindi) ambao RA anaonekana kama kinara wa maslahi yao katika ngazi ya kisiasa ingawa yyeye ni Muiran (mbulushi)zaidi ya uhindi.