Nafahamu watu wengi wamejiuliza
sana kwa nini Christiano Ronaldo alifunga magoli mawili juzi kwenye
mechi na kwenye mechi na Granada lakini hakushangilia hata kidogo kitu
ambacho sio kawaida yake.
Stori ni kwamba Ronaldo
amekubali kutoa sentensi yenye maneno machache kuhusu yeye
kutokushangilia ambapo Kauli iliyonukuliwa na Sky sports kutoka kwa
Ronaldo ni kwamba, ni kweli yuko kwenye huzuni na timu yake ya Real
Madrid inafahamu chanzo cha huzuni yake ambayo ndio sababu iliyomfanya
asishangilie wakati alipofunga magoli mawili kwenye ligi ndani ya mechi
iliyochezwa jana dhidi ya Granada.
Ungetarajia kwamba Ronaldo
angeshangilia kupitiliza juzi (september 2) kwasababu alifikisha magoli
150 kwenye mechi yake ya 149 toka ajiunge na club hiyo lakini haikua
hivyo.
Cristiano ambae miezi michache
iliyopita alinukuliwa akisema anapenda kuichezea Real Madrid kwenye
maisha yake yote yaliyobaki kwenye soka, amesema kilichomfanya asifurahi
sio ishu yake binafsi bali ni ya kikazi zaidi na hakutaka kuongeza
chochote kwenye hiyo kauli.
No comments:
Post a Comment