MWENYEKITI wa Chama cha Democratic Party (DP), Mchungaji
Christopher Mtikila, ameshinda kesi ya uchochezi iliyokuwa
inamkabili.Akizungumza baada ya kushinda kesi hiyo, Mtikila amesema,
“Ushindi huu niliutarajia maana hata asubuhi kabla ya kuja mahakamani
niliongea na Yesu na sasa amenijibu”.
Mara baada ya kushinda kesi hiyo lilizuka timbwili lingine baada ya
mtu mmoja kujitokeza akiwa na RB (Report Book) akimtuhumu Mchungaji
Mtikila kuwa alimtishia kumuua na ni mwizi wa viwanja. Baada ya kutaka
kukamatwa na polisi mmoja aliyekuwa na cheo cha Koplo, Mchungaji
alikataa kwa madai kuwa yeye ni kiongozi wa kitaifa hivyo hawezi
kukamatwa na polisi mwenye cheo cha Koplo, labda polisi mwenye cheo cha
SSP (Senior Superintendent of Police). Kwa kauli hiyo polisi alishindwa
kumtia nguvuni.
Taarifa via GPL
Taarifa via GPL
* “Hukumu dhidi ya Mwenyekiti wa Chama cha DP, Mchungaji
Christopher Mtikila, iliyoahirishwa mara mbili kwa sababu ya hakimu kuwa
na dharura, ilisomwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu a
Hakimu Mkazi Mfawidhi, Illivin Mugeta aliyeisikiliza kesi hiyo ya kutoa
maneno ya uchochezi.Mtikila alikuwa akikabiliwa na mashitaka ya
kusambaza waraka wa uchochezi dhidi ya Rais Jakaya Kikwete, kwamba
anataka kuuangamiza Ukristo.
Mshitakiwa Mtikila alifunga ushahidi kwa kuwa na mashahidi wawili wa
utetezi, akihofia kupoteza fedha za Serikali kwa kuwaleta mashahidi
wengi ambao hawana kitu tofauti na mashahidi wengine waliokuwa
wamewasilisha ushahidi wao mahakamani hapo.
Mtikila, anadaiwa kwamba, Aprili, 2010 Dar es Salaam, alisambaza waraka aliokuwa akidai ni wa kuunusuru Ukristo wenye lengo la kuangamizwa na Jihad ya Rais Jakaya Kikwete na kwamba Wakristo wajitoe mhanga kukomesha ugaidi, “Kikwete anaangamiza Ukristo, amekuwa jasiri wa kuingiza Uislamu katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alidai Mtikila katika waraka wake huo.
Alidai waraka uliosambazwa alisaini akiwa kama Mwenyekiti wa Kamati ya Kuunusuru Ukristo na walichapisha nakala 100,000, lakini aligoma kutaja mahali walipochapishia nakala hizo. Maelezo yote hayo yalitolewa mahakamani kama kielelezo na ofisa wa polisi, SSP, Ibeleze Mrema aliyemuhoji Mtikila Aprili 14, 2010.”
(* ” nukuu ya taarifa ya gazeti la MTANZANIA le leo kabla ya hukumu kusomwa)
Mtikila, anadaiwa kwamba, Aprili, 2010 Dar es Salaam, alisambaza waraka aliokuwa akidai ni wa kuunusuru Ukristo wenye lengo la kuangamizwa na Jihad ya Rais Jakaya Kikwete na kwamba Wakristo wajitoe mhanga kukomesha ugaidi, “Kikwete anaangamiza Ukristo, amekuwa jasiri wa kuingiza Uislamu katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alidai Mtikila katika waraka wake huo.
Alidai waraka uliosambazwa alisaini akiwa kama Mwenyekiti wa Kamati ya Kuunusuru Ukristo na walichapisha nakala 100,000, lakini aligoma kutaja mahali walipochapishia nakala hizo. Maelezo yote hayo yalitolewa mahakamani kama kielelezo na ofisa wa polisi, SSP, Ibeleze Mrema aliyemuhoji Mtikila Aprili 14, 2010.”
(* ” nukuu ya taarifa ya gazeti la MTANZANIA le leo kabla ya hukumu kusomwa)
No comments:
Post a Comment