Tuesday, September 18, 2012

JAMANI TUZUNGUMZE MAPENZI

Kila mtu anajua habari za mapenzi,hata wewe unayesoma habari hii unajua habari hizi. Mapenzi ni matunda matamu na pia ni matunda machungu.Sijui inategemea nini lakini nadhani ni kadri unavyoyapata,unavyoyala,na unavyojisikia wakati unaanza kula au unapomaliza.
Blog hii ni ya watu wazima,watu wanaojua nini maana ya mapenzi au wanaojaribu kujua zaidi.Nimeamua kuanzisha blogu hii kwa sababu najua ipo haja ya watu kuendelea kubadilishana mawazo juu ya mapenzi,ngono na mengineyo yanayohusiana na miili yetu,zikiwemo afya zetu.Si mnajua kwamba kitumbua siku hizi kimeingia mchanga ndugu zangu?

Kwa hiyo keti kitako tuanze kuyachambua masuala ya mapenzi. Kwa utaalamu wangu wa masuala haya nadhani nitakuwa tayari kujibu maswali yenu,hoja zenu nk kuhusiana na mapenzi,kujamiiana(ngono) na mengi mengineyo. Jisikie huru kunitumia email au kuuliza swali lako hapa hapa,nitakujibu. Lakini kwa kuanzisha hoja,hebu niambie,mapenzi ni nini kwa jinsi unavyoelewa wewe?Ni kwanini eti watu wanauana,wanafarakana,wanachinjana,nchi zinaingia kwenye vita kisa mapenzi? Je hayo yanabakia kuwa mapenzi au chuki? Kuna uhusiano gani kati ya mapenzi na wivu?Yupi ana nguvu kumshinda mwenzake?

No comments:

Post a Comment